Nigeria
Jamhuri ya Shirikisho ya Nigeria Jamhuriyar Tarayyar Najeriya (Hausa) Ọ̀hàńjíkọ̀ Ọ̀hànézè Naìjíríyà (Igbo) Orílẹ̀-èdè Olómìniira Àpapọ̀ Nàìjíríà (Yoruba) | |
|---|---|
| Kaulimbiu: Unity and Faith, Peace and Progress | |
| Wimbo wa taifa: "Nigeria, We Hail Thee" | |
| Mji mkuu | Abuja |
| Mji mkubwa | Lagos |
| Lugha rasmi | Kiingereza |
| Kabila (2018) | Hausa 30%, Yoruba 15.5%, Igbo 15.2%, Fulani 6%, wengine 33.3% |
| Serikali | Jamhuri ya kirais ya shirikisho |
• Rais | Bola Tinubu |
• Makamu wa Rais | Kashim Shettima |
• Muungano wa Nigeria | 1 Januari 1914 |
• Uhuru kutoka Uingereza | 1 Oktoba 1960 |
| Eneo | |
| • Jumla | km2 923,769 (ya ya 31) |
| • Maji (asilimia) | 1.4% |
| Idadi ya watu | |
| • Kadirio la 2023 | ▲ 236,747,130 |
| • Msongamano | 249.8/km2 |
| PLT (PPP) | Kadirio la 2024 |
| • Jumla | ▲ $1.443 trilioni (ya 27) |
| • Kwa kila mtu | ▲ $6,340 |
| PLT (Kawaida) | Kadirio la 2024 |
| • Jumla | |
| • Kwa kila mtu | |
| HDI (2022) | 0.548 chini |
| Sarafu | Naira (₦) |
| Majira ya saa | UTC+1 WAT |
| Upande wa magari | Kushoto |
| Msimbo wa simu | +234 |
| Jina la kikoa | .ng |
Nigeria pia Nijeria, rasmi kama Jamhuri ya Shirikisho ya Nigeria ni nchi iliyoko Magharibi mwa Afrika. Inapakana na Benin upande wa magharibi, Niger upande wa kaskazini, Chad na Kameruni upande wa mashariki, na upande wa kusini na Bahari ya Atlantiki. Ikiwa na idadi ya watu milioni 232 ndio nchi ya sita kubwa duniani kwa idadi ya watu na ni nchi yenye idadi kubwa zaidi ya watu barani Afrika. Abuja ndiyo mji mkuu, huku Lagos ikiwa jiji kubwa zaidi.
Nigeria imepata uhuru wake tarehe 1 Oktoba 1960, ikiunganisha maeneo ya koloni la Nigeria na sehemu ya kaskazini ya eneo lindwa la Kamerun ya Kiingereza.
Nijeria ni jamhuri ya shirikisho inayojumuisha majimbo 36 na Eneo la Mji Mkuu wa Shirikisho, ikiendesha serikali kwa mfumo wa urais. Ilipata uhuru kutoka kwa Uingereza mwaka 1960 na kuwa jamhuri mwaka 1963. Nijeria ina wakazi wa makabila mbalimbali na tamaduni tofauti, ikiwa na zaidi ya makabila 250. Makabila matatu makubwa ni Wahausa-Wafulan upande wa kaskazini, Wayoruba upande wa kusini-magharibi, na Waigbo upande wa kusini-mashariki. Kiingereza ndicho lugha rasmi, lakini lugha nyingi za asili kama vile Hausa, Wayoruba, na Igbo huzungumzwa kwa wingi nchini kote.
Nijeria ina uchumi wa 4 kwa ukubwa barani Afrika, unaoendeshwa na sekta kama mafuta na gesi, kilimo, mawasiliano ya simu, na huduma. Ni miongoni mwa wazalishaji wakuu wa mafuta duniani, ambapo mauzo ya mafuta nje yanachangia kwa kiasi kikubwa mapato ya serikali na fedha za kigeni. Hata hivyo, nchi inakabiliwa na changamoto kama vile ufisadi, ukosefu wa usalama, umaskini, na upungufu wa miundombinu. Licha ya changamoto hizo, Nijeria bado ni nguvu ya kikanda na mwanachama mwenye ushawishi katika mashirika ya kimataifa kama Umoja wa Afrika (AU), ECOWAS, na Umoja wa Mataifa.
Jiografia
[hariri | hariri chanzo]Nigeria inaunganisha maeneo tofauti sana ikiwa na msitu wa mvua upande wa kusini kupitia nchi ya savana hadi kanda ya Sahel na mwanzo wa jangwa la Sahara kaskazini kabisa.
Mlima wa juu ni Chappal Waddi yenye m 2,419 juu ya UB.
Hali ya hewa ni ya kitropiki. Kusini kuna mvua mwaka wote lakini kaskazini mwa nchi kuna ukame kati ya Novemba na Aprili.
Mito mikubwa ni mto Niger na mto Benue; yote miwili inakutana na kuishia katika delta ya Niger ambayo ni kati ya delta kubwa zaidi duniani.
Mji mkubwa zaidi ni Lagos (mji mkuu wa zamani) ukiwa na wakazi 15,000,000. Kati ya miji mingine kuna Abuja, Kano, Ibadan, Oshogbo, Ilorin, Abeokuta, Ogbomosho na Port Harcourt.

Historia
[hariri | hariri chanzo]Historia ya kale (hadi waka 1500)
[hariri | hariri chanzo]Tangu mnamo 500 KK kulikuwa na Utamaduni wa Nok kaskazini mwa Nigeria. Unajulikana tu kutokana na sanamu kubwa za watu zilizotengenezwa kwa terakota (udongo wa kuchomwa) ambazo zilitengenezwa kati ya 500 KK na 200 BK kufuatana na vipimo vya rediokaboni. [1][2][3][4]
Kumbukumbu ya mji wa Kano inaanza katika mwaka 999 BK.
Katika kusini milki ya Nri kati ya Waigbo ilianza kabla ya karne ya 10 BK ikaendelea hadi kumezwa na koloni la Uingereza mwaka 1911.[5][6] Nri ilitawaliwa na mfalme (Eze Nri) na mji wa Nri huangaliwa kama chanzo cha utamaduni wa Waigbo.[7]
Tangu karne ya 12 kuna habari za falme za Ife na Oyo katika kusini magharibi zilizoundwa na Wayoruba. [8][9] and 14th[10] Ife ilianza kukaliwa na watu tangu karne ya 9 na utamaduni wake ulitengeneza sanamu mashuhuri za terakota na bronzi. [8].
Karne za kati
[hariri | hariri chanzo]Mnamo mwaka 1500 kulikuwa na falme kubwa katika eneo la Nigeria ya leo. Katika kusini ni milki ya Benin (tofauti na nchi ya leo) na Onitsa ya Waigbo, katika kaskazini falme za Wahausa na Songhai ambazo zilitawaliwa na wafalme au masultani Waislamu. Falme za kaskazini zilishiriki katika biashara ya ng'ambo ya Sahara ambako hasa chumvi, dhahabu na watumwa walipelekwa kwa njia ya misafara hadi nchi za Waislamu karibu na Bahari Mediteranea. [11], [12]
Wakati huohuo wapelelezi Wareno na Wahispania walianza kufika kwenye pwani za Afrika ya Magharibi na pia katika delta ya Niger. Walianza kujenga vituo vya biashara kwa vibali vya watawala wa sehemu za pwani kama huko Lagos na Calabar. Wazungu walifanya biashara ya bidhaa mbalimbali na watu wa pwani na hii ilikuwa pia chanzo cha biashara ya watumwa ya kuvukia Atlantiki. [13] Bandari ya Calabar kwenye Hori ya Biafra (leo hii inajulikana zaidi kwa jina la "Bight of Bonny") iliendelea kuwa moja kati ya vituo vya biashara ya watumwa vikubwa zaidi kwenye pwani ya Afrika ya Magharibi. Vituo vingine vya biashara ya watumwa kwenye pwani ya Nigeria vilikuwa Lagos na Badagry, [13][14] Wangi waliouzwa hapo walifukuwa wafungwa wa vita vya watawala wenyeji kati yao au walikamatwa katika kampeni zilizoendeshwa kwa shabaha za kupata watumwa wa kuuzwa. [15]
Watendaji wakuu walioleta watumwa pwani walitoka katika milki ya Oyo kwenye kusini magharibi na Ukhalifa wa Sokoto katika kaskazini. [13][14]
Utumwa katika maeneo ya Nigeria ya leo haukuanzishwa na watu kutoka Ulaya, ulikuwepo tayari pia biashara ya watumwa.[16] Lakini soko jipya kwenye pwani lililoanzishwa na Wazungu lilibadilisha uwiano katika jamii nyingi za Kiafrika na pia uhusiano kati ya jamii za Kiafrika. Watawala karibu na pwani waliweza kupata faida kwa kuuza watumwa moja kwa moja kwa Wazungu na waliweza kununua silaha za moto; wenye silaha za moto waliweza kushinda vita, kupata wafungwa wengi na kuuza wafungwa wengi zaidi. Hivyo mahitaji makubwa ya soko la watumwa la Atlantiki yalilisha ufuatano wa vita na mashindano ya kukamata wafungwa zaidi.[17]
Idadi ya watumwa ndani ya Nigeria ilizidi kukua katika karne ya 19 ambako biashara ya watumwa kwenye Atlantiki ilikwisha. Manmo 1890 mkusanyiko mkubwa wa watumwa katika Afrika walikuwa watumwa katika milki ya Khalifa wa Sokoto, takriban watu milioni 2. [18]
Karne ya 19 na ukoloni
[hariri | hariri chanzo]Tangu mnamo 1860 Uingereza ilianza kupanua athira yake katika Nigeria. Uingereza ilikuwa nchi ya kwanza kuwa na viwanda vingi; viwanda vyake vilihitaji mafuta kwa matumizi ya grisi kwa kulainisha mwendo wa mashine. Delta ya mto Niger ilikuwa na idadi kubwa ya michikichi inayozalisha mafuta.[19] Hapo shirika kama Royal Niger Company zilipata maeneo makubwa chini ya mamlaka yao kwa njia ya mapatano na mikataba na watawala wenyeji, malipo na matishio na maeneo haya yaliwekwa baadaye chini ya serikali ya Uingereza.
Kwenye mkutano wa Berlin madai ya Uingereza juu ya pwani ya Nigeria yalikubaliwa na mataifa mengine ya Ulaya. Baadaye Waingereza waliendelea haraka kuhakikisha mamlaka yao juu ya maeneo ya kaskazini ama kwa mapatano au kwa vita kwa kusudi la kuzuia upanuzi wa Ufaransa.
Hivyo zilitokea maeneo ya "Southern Nigeria Protectorate" na "Northern Nigeria Protectorate". Hali halisi sehemu hizi haziwahi kuwa na umoja katika historia lakini hatimaye Uingereza iliamua kutawala maeneo yote kama koloni moja.
Baada ya uhuru
[hariri | hariri chanzo]Nigeria ilipata uhuru wake tarehe 1 Oktoba 1960 kutoka kwa Uingereza ikiunganisha maeneo ya koloni la Nigeria na sehemu ya kaskazini ya eneo lindwa la Kamerun ya Kiingereza.
Kati ya miaka 1967-1970 nchi iliona vita ya wenyewe kwa wenyewe; magharibi ya nchi, inayokaliwa na Waigbo hasa, ilijaribu kujitenga kwa jina la Biafra, ikipinga utawala wa wanajeshi Waislamu. Takriban watu milioni 2 walikufa kwa njaa wakati ule.
Nigeria iliendelea kuvurugika na mapinduzi ya kijeshi.
Tangu miaka ya 1970 Nigeria ilikuwa na mapato makubwa kutokana na mafuta yaliyotolewa kutoka ardhi yake, hasa katika delta ya mto Niger.
Ulaji rushwa na ufisadi wa watawala wa kijeshi ulizuia maendeleo ya nchi jinsi ilivyoonekana katika nchi nyingine yenye mafuta.
Tangu mwaka 1999 nchi imerudi kwenye utawala wa kisheria ikapata katiba mpya na kumchagua rais Olusegun Obasanjo aliyerudishwa madarakani mara moja.
Majaribio ya wafuasi wake wa kubadilisha katiba na kumpa kipindi cha tatu yalishindikana bungeni.
Katika uchaguzi wa mwaka 2007 Umaru Yar’Adua alishinda kwa asilimia 70 za kura.
Baada ya kungonjeka kwake, makamu wa rais Goodluck Jonathan alichukua madaraka ya urais kuanzia mwaka 2010 akachaguliwa kuwa rais kwenye kura ya mwaka 2011.
Mwaka 2015 alishindwa katika uchaguzi mkuu na mgombea mwenzake, Muhammadu Buhari.
Ni kwamba tangu mwaka 2009 hadi Septemba 2015 uasi wa kundi la Boko Haram ulivuruga amani na usalama nchini Nigeria. Wanamgambo wa kundi hilo wanaotazamwa na Wanigeria wengi kuwa magaidi walianza kutwaa mamlaka juu ya sehemu za nchi hasa katika mazingira ya jimbo la Borno, kuua wananchi wengi, kuchukua watu mateka na kupigana na jeshi la Nigeria na ya nchi jirani.
Kutofaulu kwa jeshi la taifa kumaliza ghasia hizo ndiyo sababu muhimu ya kushindwa kwa rais Jonathan kwenye uchaguzi wa mwaka 2015. Kufuata na ahadi zake kwa wapiga kura, Muhammadu Buhari alijitahidi kukomesha kundi hilo.
Jeshi
[hariri | hariri chanzo]Jeshi la Nigeria lina jukumu la kulinda Jamhuri ya Shirikisho ya Nigeria, kukuza maslahi ya usalama wa kimataifa ya Nigeria, na kuunga mkono juhudi za kulinda amani hasa katika Afrika Magharibi.
Jeshi la Nigeria linaundwa na Jeshi la Ardhi, ni Jeshi la Wanamaji na Jeshi la Anga. Jeshi nchini Nigeria limecheza jukumu kubwa katika historia ya nchi tangu uhuru. Junta mbalimbali zilikamata udhibiti wa nchi na zilitawala kupitia wengi wa historia yake.
Kipindi cha mwisho cha utawala wake kilimalizika mwaka 1999 kufuatia kifo cha ghafla cha dikteta wa zamani Sani Abacha mwaka 1998, na mrithi wake, Abdulsalam Abubakar, kumpa mamlaka ya serikali Olusegun Obasanjo aliyechaguliwa kidemokrasia mwaka wa 1999.
Ikichukua faida ya jukumu lake kama nchi yenye wakazi wengi wa Afrika, Nigeria imeweka jeshi lake kama kikosi cha kulinda amani Afrika. Tangu mwaka 1995, jeshi la Nigeria, kupitia mamlaka ya ECOMOG, limetumwa kulinda amani katika Liberia (1997), Ivory Coast (1997-1999), Sierra Leone 1997-1999, na kwa sasa katika mkoa wa Darfur huko Sudan chini ya Umoja wa Afrika.
Uchumi
[hariri | hariri chanzo]
Nigeria ina mojawapo ya uchumi mkubwa zaidi barani Afrika na inaainishwa kama uchumi mchanganyiko wa kipato cha chini cha kati. [20] Muundo wake wa kiuchumi unategemea sana sekta rasmi na isiyo rasmi, ukiwa na mchango mkubwa kutoka mafuta na gesi, kilimo, huduma, na biashara. Uchumi huathiriwa na mabadiliko ya bei za mafuta duniani, thamani ya sarafu, na changamoto za kimuundo za ndani, hali inayobadilisha nafasi yake ya Pato la Taifa ikilinganishwa na nchi nyingine kubwa za Afrika kama Afrika Kusini na Misri. [21]
Sekta ya mafuta ya petroli bado ni sehemu muhimu ya uchumi, ikichangia sehemu kubwa ya mapato ya mauzo ya nje na mapato ya serikali. [22] Nigeria ni mwanachama wa OPEC na huzalisha mafuta ghafi hasa katika eneo la Delta ya Niger. Hata hivyo, sekta zisizo za mafuta zimeongezeka umuhimu, hasa kilimo, mawasiliano ya simu, na huduma za kifedha. [23] Kilimo huajiri sehemu kubwa ya watu na kinajumuisha uzalishaji wa mazao kama muhogo, mahindi, viazi vikuu, kakao, na mpunga, pamoja na ufugaji wa mifugo. [24]
Sekta ya huduma imepanuka kwa kiasi kikubwa, hasa katika benki, teknolojia ya fedha, na huduma za kidijitali, ambapo Lagos hutumika kama kituo kikuu cha kiuchumi na kifedha katika Afrika Magharibi. [25] Nigeria pia ina sekta kubwa ya viwanda na biashara isiyo rasmi inayosaidia matumizi ya ndani na ajira. Uchumi wake una soko kubwa la ndani kutokana na idadi ya watu inayozidi milioni 200, na kuifanya kuwa moja ya nchi zenye watu wengi zaidi duniani. [26]
Biashara ya kimataifa inatawaliwa na mauzo ya nje ya mafuta ghafi, huku bidhaa zinazoagizwa kutoka nje zikiwa ni mafuta yaliyosafishwa, mashine, magari, na bidhaa za matumizi ya kila siku. [27] Nigeria ni mwanachama wa ECOWAS na Umoja wa Afrika, taasisi zinazosaidia ushirikiano wa kikanda na uratibu wa biashara. [28] Licha ya ukubwa wa uchumi wake na utajiri wa rasilimali, nchi inaendelea kukabiliwa na changamoto za kimuundo kama mfumuko wa bei, ukosefu wa ajira, upungufu wa miundombinu, na utegemezi mkubwa wa mapato ya mafuta. [29]
Demografia
[hariri | hariri chanzo]Nigeria hukadiriwa kuwa na wakazi takriban milioni 180. Inasemekana nusu ya wakazi wote wana umri wa chini ya miaka 14. Hata hivyo ni vigumu kupata namba halisi kwa sababu ya umuhimu wake katika siasa.
Vikundi vikubwa katika jumla la makabila 300 ni Wahausa na Wafula kaskazini (jumla 20-30%), Waigbo (Waibo) kusini (14-18%), Wayoruba katika sehemu za magharibi (20-27%).
Katika miji mikubwa watu kukaa kwa mchanganyiko wa makabila.
Nigeria iliona mara kadhaa vurugu na mapambano kati ya makabila yaliyoongezewa ukali kwa sababu mara nyingi ukabila unaendelea sambamba na udini. Watu wa Kaskazini ni Waislamu zaidi na watu wa kusini Wakristo zaidi.
Dini
[hariri | hariri chanzo]
Kuthibitisha idadi ya wafuasi wa dini mbalimbali ni vigumu vilevile. Kwa ujumla kaskazini ya nchi ina historia ndefu ya Uislamu na wakazi ni Waislamu, hasa Wahausa. Kusini kuna Wakristo wengi, Waigbo ni zaidi Wakatoliki na Wayoruba zaidi Waprotestanti.
Wengi wanasema ya kwamba idadi za Wakristo na za Waislamu zinalingana - wengine wanaona Waislamu ni wengi kidogo labda 50%, Wakristo 40% na wafuasi wa dini asilia za Kiafrika takriban 10%, lakini hawa wa mwisho kwa sasa wamepungua sana, labda wamebaki 1.4%.
Kati ya Waislamu, wengi ni Wasuni. Kati ya Wakristo, 74% ni Waprotestanti na 25% ni Wakatoliki.
Tangu mwaka 1999 suala la sharia au sheria za Kiislamu limeleta utata na mapambano katika majimbo kadhaa. Jimbo la Zamfara linalokaliwa hasa na Wahausa ambao ni Waislamu liliamua kuwa na sharia kama sheria ya kijimbo mwaka 1999 na majimbo mengine yalifuata. Kwa sasa ni Kano, Katsina, Niger, Bauchi, Borno, Kaduna, Gombe, Sokoto, Jigawa, Yobe na Kebbi. Kanuni za sharia hazitumiwi kwa namna moja kati ya majimbo haya; mapambano yalitokea juu ya jinsi gani sharia inaathiri raia wasio Waislamu.
Lugha rasmi ya nchi ni Kiingereza, ingawa wakazi wengi wanatumia zaidi lugha za makabila yao, ambayo ni zaidi ya 500. Muhimu zaidi ni Kihausa, Kiigbo na Kiyoruba.
Serikali na Utawala
[hariri | hariri chanzo]Serikali ya Nigeria imepangwa kama jamhuri ya shirikisho yenye rais wa mfumo wa kikatiba, ambapo mamlaka ya kiutendaji yametenganishwa na majukumu ya bunge na mahakama chini ya Katiba ya 1999 iliyofanyiwa marekebisho. [30] Rais wa Nigeria hutumika kama mkuu wa nchi na mkuu wa serikali na huchaguliwa kwa kura za wananchi kwa muda wa juu ya mihula miwili ya miaka minne kila moja. [31] Rais huongoza Baraza la Shirikisho la Utendaji, huteua mawaziri, na anawajibika kutekeleza sera za kitaifa, kusimamia taasisi za shirikisho, na kusimamia utawala wa umma.
Tawi la kutunga sheria la serikali ni Bunge la taifa, ambalo lina mabunge mawili yanayojumuisha Seneti na Baraza la Wawakilishi. [32] Seneti inawakilisha majimbo kwa usawa, wakati Baraza la Wawakilishi linategemea mgawanyo wa idadi ya watu katika maeneo bunge ya shirikisho. Bunge la taifa lina jukumu la kutunga sheria za shirikisho, kuidhinisha bajeti, na kusimamia utendaji wa tawi la kiutendaji. Katika ngazi ya chini, Nigeria imegawanywa katika majimbo 36 na Eneo la Mji Mkuu wa Shirikisho, kila moja ikiwa na gavana na bunge la jimbo linalosimamia utawala wa kikanda. [33]
Mfumo wa mahakama wa Nigeria ni huru na unaongozwa na Mahakama ya Juu, ambayo ndiyo mahakama ya juu zaidi nchini. [34] Mahakama nyingine muhimu ni Mahakama ya Rufaa na Mahakama Kuu za Shirikisho, pamoja na mahakama za ngazi ya majimbo. Mahakama hutafsiri sheria, kutatua migogoro, na kuhakikisha ufuataji wa katiba katika taasisi za serikali. Uongozi wa mahakama hupangwa kupitia uteuzi unaofanywa na Rais kwa mapendekezo ya mabaraza ya mahakama, ukihitaji pia idhini ya bunge katika baadhi ya hali. [35]
Mfumo wa utawala wa Nigeria pia unajumuisha serikali za mitaa (LGAs), ambazo hushughulikia utawala wa ngazi ya chini kama miundombinu ya msingi, msaada wa elimu ya msingi, na huduma za maendeleo ya eneo. [36] Uongozi katika ngazi zote hufanya kazi ndani ya mfumo wa shirikisho, ambao unasambaza madaraka kati ya serikali ya taifa, majimbo, na serikali za mitaa. Mfumo huu umeundwa kusimamia idadi kubwa ya watu wa Nigeria, utofauti wa kikabila, na tofauti za kikanda huku ukidumisha umoja wa kitaifa na uratibu wa kiutawala. [31]
Majimbo ya shirikisho
[hariri | hariri chanzo]
Muundo wa Nigeria ni Jamhuri ya Shirikisho. Katiba ya nchi imefuata mfano wa katiba ya Marekani.
Rais huchaguliwa na wananchi wote: ndiye mkuu wa serikali. Anawajibika mbele ya bunge lenye vitengo viwili: Senati na Baraza la Wawakilishi.

Tazama pia
[hariri | hariri chanzo]Marejeo
[hariri | hariri chanzo]- ↑ Nicole Rupp, Peter Breunig & Stefanie Kahlheber, "Exploring the Nok Enigma", Antiquity 82.316, June 2008.
- ↑ B. E. B. Fagg, "The Nok Culture in Prehistory", Journal of the Historical Society of Nigeria 1.4, December 1959.
- ↑ Kleiner, Fred S.; Christin J. Mamiya (2009). Gardner's Art Through the Ages: Non-Western Perspectives (tol. la 13, revised). Cengage Learning. uk. 194. ISBN 0-495-57367-1.
- ↑ "Nok Terracottas (500 B.C.–200 A.D.) | Thematic Essay | Heilbrunn Timeline of Art History | The Metropolitan Museum of Art". Metmuseum.org. 2014-06-02. Iliwekwa mnamo 2014-07-16.
- ↑ Juang, Richard M. (2008). Africa and the Americas: culture, politics, and history : a multidisciplinary encyclopedia, Volume 2. ABC-CLIO. uk. 597. ISBN 1-85109-441-5.
- ↑ Hrbek, Ivan (1992). Africa from the seventh to the eleventh Century. James Currey Publishers. uk. 254. ISBN 0-85255-093-6.
- ↑ Uzukwu, E. Elochukwu (1997). Worship as Body Language. Liturgical Press. uk. 93. ISBN 0-8146-6151-3.
- 1 2 Falola, Toyin; Heaton, Matthew M. (2008). A history of Nigeria. Cambridge University Press. uk. 23. ISBN 0-521-68157-X.
- ↑ Laitin, David D. (1986). Hegemony and culture: politics and religious change among the Yoruba. University of Chicago Press. uk. 111. ISBN 0-226-46790-2.
- ↑ MacDonald, Fiona; Paren, Elizabeth; Shillington, Kevin; Stacey, Gillian; Steele, Philip (2000). Peoples of Africa, Volume 1. Marshall Cavendish. uk. 385. ISBN 0-7614-7158-8.
- ↑ Ralph A. Austen, Trans-Saharan Africa in World History, Oxford University Press, 2010 , uk. 26 (imeangaliwa kupitia google books, tar. 3-12-2016
- ↑ Ghislaine Lydon, On Trans-Saharan Trails: Islamic Law, Trade Networks, and Cross-Cultural Exchange in Nineteenth-Century Western Africa uk. 85f; Cambridge University Press, 2009 ; imeangaliwa kupitia google books 3-12-2016
- 1 2 3 Gordon, April A. (2003). Nigeria's Diverse Peoples: A Reference Sourcebook. ABC-CLIO. ku. 44–54. ISBN 1576076822. Iliwekwa mnamo 2015-03-29.
- 1 2 Falola, Toyin; Genova, Ann (2009). Historical Dictionary of Nigeria. Scarecrow Press. uk. 328. ISBN 0810863162. Iliwekwa mnamo 2015-03-29.
- ↑ Falola, Toyin; Paddock, Adam (2012). Environment and Economics in Nigeria. Routledge. uk. 78. ISBN 1136662472. Iliwekwa mnamo 2015-03-29.
- ↑ "Slavery – Historical survey – Slave societies". Encyclopædia Britannica's Guide to Black History. Encyclopædia Britannica. 2011. Iliwekwa mnamo 28 Mei 2011.
{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link) - ↑ Nigeria's Diverse Peoples: A Reference Sourcebook von April A. Gordon, uk. 49
- ↑ "It is estimated that by the 1890s the largest slave population of the world, about 2 million people, was concentrated in the territories of the Sokoto Caliphate. The use of slave labor was extensive, especially in agriculture."Kevin Shillington (2005). Encyclopedia of African History. Michigan University Press. p. 1401. ISBN 1-57958-455-1
- ↑ S.O. Aghalino, British colonial policies and the oil palm industry in the Niger delta region of Nigeria Ilihifadhiwa 16 Januari 2013 kwenye Wayback Machine., African Study Monographs, 21(1): 19-33, January 2000, tovuti ya Chuo Kikuu cha Kyoto, iliangaliwa 3-12-2016
- ↑ "Nigeria Economic Overview". worldbank.org. World Bank. Aprili 2026. Iliwekwa mnamo Mei 8, 2026.
{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link) - ↑ "World Economic Outlook Database: April 2026". IMF.org. International Monetary Fund. Aprili 14, 2026. Iliwekwa mnamo Mei 8, 2026.
{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link) - ↑ "Nigeria: Member Country". opec.org. Organization of the Petroleum Exporting Countries. 2024. Iliwekwa mnamo Mei 8, 2026.
{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link) - ↑ Reuben Kenrick Udo (Aprili 15, 2026). "Economy of Nigeria". Britannica. Iliwekwa mnamo Mei 8, 2026.
{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link) - ↑ "Nigeria at a glance". fao.org. Food and Agriculture Organization of the United Nations. 2024. Iliwekwa mnamo Mei 8, 2026.
{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link) - ↑ "Nigeria: Major Economic Highlights". Coface. 2025. Iliwekwa mnamo Mei 8, 2026.
{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link)[dead link] - ↑ "United Nations Country Profile: Nigeria". un.org. United Nations Statistics Division. 2024. Iliwekwa mnamo Mei 8, 2026.
{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link) - ↑ "Nigeria - World Factbook: Economy". cia.gov. Central Intelligence Agency. Aprili 28, 2026. Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2021-01-09. Iliwekwa mnamo Mei 8, 2026.
{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link) - ↑ "Member State Profile: Nigeria". au.int. African Union. 2024. Iliwekwa mnamo Mei 8, 2026.
{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link)[dead link] - ↑ "Nigeria Economic Outlook". afdb.org. African Development Bank. 2024. Iliwekwa mnamo Mei 8, 2026.
{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link) - ↑ "The Government of Nigeria". nigeria.gov.ng. Federal Government of Nigeria. 2024. Iliwekwa mnamo Mei 9, 2026.
{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link)[dead link] - 1 2 Reuben Kenrick Udo (Aprili 15, 2026). "Nigeria: Government and society". Britannica. Iliwekwa mnamo Mei 9, 2026.
{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link) - ↑ "History of the National Assembly". nass.gov.ng. National Assembly of Nigeria. 2024. Iliwekwa mnamo Mei 9, 2026.
{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link) - ↑ "Nigeria's Political System". CFR.org. Council on Foreign Relations. 2024. Iliwekwa mnamo Mei 9, 2026.
{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link)[dead link] - ↑ "About the Supreme Court of Nigeria". supremecourt.gov.ng. 2024. Iliwekwa mnamo Mei 9, 2026.
{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link) - ↑ "National Judicial Council of Nigeria". njc.gov.ng. 2024. Iliwekwa mnamo Mei 9, 2026.
{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link) - ↑ "The Local Government System in Nigeria" (PDF). clgf.org.uk. Commonwealth Local Government Forum. 2024. Iliwekwa mnamo Mei 9, 2026.
{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link)
Viungo vya nje
[hariri | hariri chanzo]- Official website
- Wikimedia Atlas of Nigeria
media kuhusu Banknotes of Nigeria pa Wikimedia Commons- Nigeria entry at The World Factbook
| Abia | Abuja Federal Capital Territory | Adamawa | Akwa Ibom | Anambra | Bauchi | Bayelsa | Benue | Borno | Cross River | Delta | Ebonyi | Edo | Ekiti | Enugu | Gombe | Imo | Jigawa | Kaduna | Kano | Katsina | Kebbi | Kogi | Kwara | Lagos | Nasarawa | Niger | Ogun | Ondo | Osun | Oyo | Plateau | Rivers | Sokoto | Taraba | Yobe | Zamfara | |
| Nchi za Afrika | |
|---|---|
| Afrika ya Kati (Jamhuri ya) | Afrika Kusini | Algeria | Angola | Benin | Botswana | Burkina Faso | Burundi | Cabo Verde | Chad | Cote d'Ivoire | Eritrea | Eswatini | Ethiopia | Gabon | Gambia | Ghana | Guinea | Guinea Bisau | Guinea ya Ikweta | Jibuti | Kamerun | Kenya | Komori | Kongo (Jamhuri ya) | Kongo (Jamhuri ya Kidemokrasia ya) | Lesotho | Liberia | Libya | Madagaska | Malawi | Mali | Misri | Morisi (Visiwa vya) | Mauritania | Moroko | Msumbiji | Namibia | Niger | Nigeria | Rwanda | Sahara ya Magharibi | Sao Tome na Principe | Senegal | Shelisheli | Sierra Leone | Somalia | Sudan | Sudan Kusini | Tanzania | Togo | Tunisia | Uganda | Zambia | Zimbabwe | |
| Maeneo ya Afrika ambayo ni sehemu za nchi nje ya Afrika | |
| Hispania: Kanari · Ceuta · Melilla | Italia: Pantelleria · Pelagie | Ufaransa: Mayotte · Réunion | Uingereza: · St. Helena · Diego Garcia | Ureno: Madeira | |
| Makala hii kuhusu maeneo ya Nigeria bado ni mbegu. Je unajua kitu kuhusu Nigeria kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni? Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |
